McCarthy: Mourinho ndiye afaaye Man Utd
Kuna uwezekano mkubwa Mourinho akamrithi Van Gaal Manchester United
Jose Mourinho ndiye
afaaye zaidi kusaidia Manchester United kukabiliana vilivyo na
Manchester City watakaokuwa chini ya Pep Guardiola msimu ujao, haya kwa
mujibu wa mshambuliaji wa zamani wa Porto Benni McCarthy.
McCarthy, 38, alicheza chini ya Mourinho raia huyo wa Ureno alipokuwa mkufunzi wa Porto.
"Mourinho ni mmoja wa watu wanaojua jinsi ya kumshinda Guardiola na mbinu zake,” ameambia BBC Sport.
- Manchester United yazungumza na Mourinho
- Van Gaal akanusha uvumi kuhusu Mourinho
- Guardiola kuwa meneja Manchester City
Guardiola, alikuwa kocha wa Barcelona, kwa sasa ni mkufunzi mkuu wa Bayern Munich.
Klabu ya Manchester City ilitangaza majuzi kwamba atamrithi Manuel Pellegrini majira yajayo ya joto.
Alifutwa kazi miezi saba tu baada ya kuongoza klabu hiyo kushinda Ligi ya Premia.
Alikuwa Chelsea kwa kipindi cha kwanza 2004-2007.
No comments:
Post a Comment