Everton
inayodhaminiwa na SportPesa imeonyesha imepania kujiimarisha msimu ujao
baada ya kumwaga pauni million 30 kumnasa beki kisiki Michael Keane kwa
mkataba wa miaka mitano.
Keane
alikuwa kisiki katika kikosi cha Burnley na klabu kadhaa kubwa
zilionekana kumtolea “mimacho” lakini Everton imefanya kweli mapemaa.
Maana
yake, Keane atakuwa kati ya wachezaji watakaotua nchini na kucheza
mechi ya kirafiki dhidi ya Gor Mahia Alhamisi ya Julai 13 kwenye Uwanja
wa Taifa jijini Dar es Salaam.
No comments:
Post a Comment