Na Kassim Mtolea,Mwanza
Timu ya soka ya Alliance ya Mkoani Mwanza imeagwa rasmi na Mkurugenzi wa timu hiyo James Bwire pamoja na Mwenyekiti wa Chama cha soka mkoani hapa(MZFA) Jackson Songora.
Akizungumza na Mpenja blog,Mkurugenzi wa timu ya Alliance James Bwire amesema kuwa maandalizi yao yapo vyema na timu itasafiri ijumaa kuelekea Manyara
Bwire alisema pia timu yao itaondoka na wachezaji 30,makocha watatu,viongozi wawili kutoka chama cha soka mkoani Mwanza,wapishi
wawili Kwa upande wa Mwenyekiti wa MZFA,Jackson songora amesema kuwa anaiomba
timu ya Alliance ifanye vyema ili ipande kuelekea ligi Daraja la pili.
Alliance FC imefanikiwa kusajili wachezaji watano kutoka timu ya Nyange na Nyamagana FC ambao ni George Philemon,Juma Mussa,Baraka
Abeid,Salim Juma na Amir Mohamed Kwa upande wake kocha wa Alliance,Kessy Mziray amesema maandalizi yao
yako vyema kwa kuwa wameweza kucheza mech tatu za kirafiki na kushinda zote.
Mechi ya Kwanza Alliance fc itacheza siku ya jumapili dhidi ya timu ya Bariadi FC kutoka Shinyanga
Alliance fc itaondoka mwanza siku ya ijumaa asubuhi kuelekea Manyara.
Timu ya soka ya Alliance ya Mkoani Mwanza imeagwa rasmi na Mkurugenzi wa timu hiyo James Bwire pamoja na Mwenyekiti wa Chama cha soka mkoani hapa(MZFA) Jackson Songora.
Akizungumza na Mpenja blog,Mkurugenzi wa timu ya Alliance James Bwire amesema kuwa maandalizi yao yapo vyema na timu itasafiri ijumaa kuelekea Manyara
Bwire alisema pia timu yao itaondoka na wachezaji 30,makocha watatu,viongozi wawili kutoka chama cha soka mkoani Mwanza,wapishi
wawili Kwa upande wa Mwenyekiti wa MZFA,Jackson songora amesema kuwa anaiomba
timu ya Alliance ifanye vyema ili ipande kuelekea ligi Daraja la pili.
Alliance FC imefanikiwa kusajili wachezaji watano kutoka timu ya Nyange na Nyamagana FC ambao ni George Philemon,Juma Mussa,Baraka
Abeid,Salim Juma na Amir Mohamed Kwa upande wake kocha wa Alliance,Kessy Mziray amesema maandalizi yao
yako vyema kwa kuwa wameweza kucheza mech tatu za kirafiki na kushinda zote.
Mechi ya Kwanza Alliance fc itacheza siku ya jumapili dhidi ya timu ya Bariadi FC kutoka Shinyanga
Alliance fc itaondoka mwanza siku ya ijumaa asubuhi kuelekea Manyara.
No comments:
Post a Comment