Wakala wa nahodha na kiungo wa timu ya taifa ya Ivory Coast, Yaya Touré Gnégnéri amethibitisha taarifa za uhakika wa mchezaji huyo kuchana na klabu ya Man City, mwishoni mwa msimu huu.
Dimitri Seluk wakala wa kiungo huyo anayeonekana kuwa nguzo muhimu katika kikosi cha Man City, amekiambia kituo cha televisheni cha Sky Sports kwamba kuna asilimia 90 kwa Toure kuondoka Etihad Stdium.
Seluk hakusema ni wapi Toure, atapoelekea endapo atakamilisha mipango ya kuondoka mjini Manchester, lakini amesisitiza suala la mchezaji wake kuhitaji kubadili mazingira ya soka lake ambalo amelicheza akiwa nchini England kuanzia mwaka 2010.
Hata hivyo inadaiwa kwamba tayari klabu tatu barani Ulaya zimeonyesha nia ya kutaka kumsajili Toure.
Yaya Toure akiwa na wakala wake Dimitri Seluk
Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 31, hakuwa na mafanikio makubwa msimu huu, kama ilivyokua misimu kadhaa iliyopita, na imebainika kuna baadhi ya mambo hayamfurahishi.
Vyombo vya habari nchini Italia, jana viliripoti kwamba uongozi wa klabu ya Inter Milan umeahidi kuyafanyia kazi mapendekezo ya meneja wa klabu hiyo kwa sasa Roberto Mancini ambaye ameonyesha dhamira ya dhati ya kumsajili Yaya Toure.
Mancini alimsajili Toure mwaka 2010, akitokea nchini Hispania alipokua akiitumikia klabu ya Barcelona kwa ada ya uhamisho wa paund million 24.
Dimitri Seluk wakala wa kiungo huyo anayeonekana kuwa nguzo muhimu katika kikosi cha Man City, amekiambia kituo cha televisheni cha Sky Sports kwamba kuna asilimia 90 kwa Toure kuondoka Etihad Stdium.
Seluk hakusema ni wapi Toure, atapoelekea endapo atakamilisha mipango ya kuondoka mjini Manchester, lakini amesisitiza suala la mchezaji wake kuhitaji kubadili mazingira ya soka lake ambalo amelicheza akiwa nchini England kuanzia mwaka 2010.
Hata hivyo inadaiwa kwamba tayari klabu tatu barani Ulaya zimeonyesha nia ya kutaka kumsajili Toure.

Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 31, hakuwa na mafanikio makubwa msimu huu, kama ilivyokua misimu kadhaa iliyopita, na imebainika kuna baadhi ya mambo hayamfurahishi.
Vyombo vya habari nchini Italia, jana viliripoti kwamba uongozi wa klabu ya Inter Milan umeahidi kuyafanyia kazi mapendekezo ya meneja wa klabu hiyo kwa sasa Roberto Mancini ambaye ameonyesha dhamira ya dhati ya kumsajili Yaya Toure.
Mancini alimsajili Toure mwaka 2010, akitokea nchini Hispania alipokua akiitumikia klabu ya Barcelona kwa ada ya uhamisho wa paund million 24.
No comments:
Post a Comment