Thursday, May 7, 2015

MWADUI FC YAVUNJA UKIMYA JUU YA KOCHA WAO

Uongozi wa timu ya Mwadui ya mkoani Shinyanga umefunguka juu ya taarifa za kuachana na kocha wake.
Taarifa mbalimbali zilidai kuwa kuna uwezekano wa wageni hao kwenye ligi kuu msimu ujao kuachana na Jamhuri kiwelu na kusaka kocha mwingine.
Lakini Mpenja blog ilibisha hodi kwenye mgodi huo wa almasi na kuzungumza na katibu kuu wa timu hiyo Ramadhani Kilao ili kujua ukweli na undani wa taarifa hiyo, ambapo katibu huyo alikanusha taarifa hizo.
"Hizi taarifa hata sijui zinatokea wapi,kwetu hatuna hizo taarifa lakini nashangaa kuona zinazungumzwa kila siku,Julio ni kocha wetu labda yeye atuache ".Alisema Kilao.
Alipoulizwa kuhusiana na taarifa za kuwepo mpango wa kuleta kocha wa kigeni,katibu huyo amesema hawajalifikiria hilo lakini alidai kwamba uwezo wanao wa kumchukua kocha yeyote awe wa ndani au nje ya nchi.
"Uwezo wa kuleta kocha tunao tena hata tukitaka watatu,lakini kwasasa hilo hatujalifikiri"Alisema.
Kocha mkuu wa Mwadui Jamhuri kiwelu alifanikiwa kuipandisha daraja timu hiyo na baada ya kufanya hivyo aliekea kukinoa kikosi kama kocha msaidizi wa muda lakini baada ya kuondoka kwa kocha James Nandwa kikosini hapo Julio sasa ndiye kocha mkuu wa wagasi wa kaya Coastal Union.

No comments:

Post a Comment

-------------------------------------------------------

-------------------------------------------------------
HABARI MPYAMPYAhttp://2.bp.blogspot.com/-mFnDPXvIysA/VOZH1z-2rpI/AAAAAAAAADs/shOR30FtkF4/s1600/anigif.gif