Thursday, May 7, 2015

CHEKI ALICHOSEMA PEP GUADIOLA BAADA YA MCHEZO WA JANA


Uwezo wa Lionel Messi ndio uliamua matokeo ya mchezo wa jana kati ya Barcelona and Bayern Munich, mchezo ambao ilishuhudiwa Bayern ambao ni mabingwa wa Ujerumani wakipokea kipigo cha mabao 3-0 katika uwanja wa Camp Nou. Hayo ni maneno ya Pep Guardiola ambaye ni kocha wa zamani wa Barcelona.
Messi alifunga magoli mawili katika mchezo huo huku akitoa pasi ya bao la mwisho lililofungwa na Mbrazil Neymar Santos Jr.
"Bayern wamefanya vizuri kwa kipindi kirefu sana," alisema Guardiola ambaye aliifunika Barca kwa umiliki wa mpira, kitu ambacho ni adimu sana kutokea kwa Barca, wachambuzi wa masuala ya soka wanasema kuwa mara ya mwisho hali hiyo kutokea kwa Barca ni mwaka 2006, alisema. 
"Lakini Messi alionesha ubora wake. Barca sio sana kivile, ila yeye si wa kawaida, Barca ni timu imara ambayo ina nyota wengine wazuri kama vile Luis Suarez na Neymar.
"Barca ni wazuri mno, wana uwezo wa kutengeneza nafasi popote watakapo. Ni vipaji vya wachezaji wao ndio vilitupoteza, kucheza hapa Camp Nou ni vigumu sana.
"Lakini hata hivyo nadhani tuliuweka mpira katika himaya yetu, mapaka pale walipopata goli lao la kwanza. Ni baada ya pale ndipo tulipoanza kupoteana, lakini sitalaumu mchezaji yeyote yule, timu imepitia vipindi vigumu sana msimu huu."

No comments:

Post a Comment

-------------------------------------------------------

-------------------------------------------------------
HABARI MPYAMPYAhttp://2.bp.blogspot.com/-mFnDPXvIysA/VOZH1z-2rpI/AAAAAAAAADs/shOR30FtkF4/s1600/anigif.gif