Uwezo
wa Lionel Messi ndio uliamua matokeo ya mchezo wa jana kati ya
Barcelona and Bayern Munich, mchezo ambao ilishuhudiwa Bayern ambao ni
mabingwa wa Ujerumani wakipokea kipigo cha mabao 3-0 katika uwanja wa
Camp Nou. Hayo ni maneno ya Pep Guardiola ambaye ni kocha wa zamani wa
Barcelona.
Messi alifunga magoli mawili katika mchezo huo huku akitoa pasi ya bao la mwisho lililofungwa na Mbrazil Neymar Santos Jr.
"Bayern
wamefanya vizuri kwa kipindi kirefu sana," alisema Guardiola ambaye
aliifunika Barca kwa umiliki wa mpira, kitu ambacho ni adimu sana
kutokea kwa Barca, wachambuzi wa masuala ya soka wanasema kuwa mara ya
mwisho hali hiyo kutokea kwa Barca ni mwaka 2006, alisema.
"Lakini
Messi alionesha ubora wake. Barca sio sana kivile, ila yeye si wa
kawaida, Barca ni timu imara ambayo ina nyota wengine wazuri kama vile
Luis Suarez na Neymar.
"Barca
ni wazuri mno, wana uwezo wa kutengeneza nafasi popote watakapo. Ni
vipaji vya wachezaji wao ndio vilitupoteza, kucheza hapa Camp Nou ni
vigumu sana.
"Lakini
hata hivyo nadhani tuliuweka mpira katika himaya yetu, mapaka pale
walipopata goli lao la kwanza. Ni baada ya pale ndipo tulipoanza
kupoteana, lakini sitalaumu mchezaji yeyote yule, timu imepitia vipindi
vigumu sana msimu huu."
No comments:
Post a Comment