Thursday, May 7, 2015

HIZI NDIZO TAARIFA SAHIHI ZA TIMU ALIKOENDA MSUVA KUFANYA MAJARIBIO


Jana habari mbalimbali za Msuva kusepa kwenda kufanya majaribio ya kucheza na soka huko South Africa zilisambaa sana. Kutoka kwenye vyanzo vyangu nililiripotu kama tetesi lakini leo asubuhi nimewasiliana na Msuva mwenyewe akiwa South Africa kupata uhakika zaidi.
Majibu ni kwamba hajaenda kufanya majaribio na Orlando Pirates, timu aliyoenda kufanya nayo majaribio ni Bidvest Wits ambayo pia inashiriki ligi kuu ya South Africa.
Bidvest Wits kwa sasa ipo namba 4 nyuma ya Pirates kwenye msimamo wa ligi. Msuva alipata nafasi pia ya kuangalia mechi kali kati ya Kaizer Chiefs vs Bidvest Wits. Hapo chini kuna audio ya sauti nikiongea nae pamoja na picha akiwa uwanjani kuangalia mechi.



Huyo jamaa aliyekaa na Msuva anaitwa Charles ndie aliyemuunganishia mchongo wa trial

BY MBEGEZE

No comments:

Post a Comment

-------------------------------------------------------

-------------------------------------------------------
HABARI MPYAMPYAhttp://2.bp.blogspot.com/-mFnDPXvIysA/VOZH1z-2rpI/AAAAAAAAADs/shOR30FtkF4/s1600/anigif.gif